Saturday 28 February 2015

HISTORIYA YA LUGHA YA KISWAHILI

Lugha ya Kiwsahili ni lugha ambayo historia yake inamjada  na mvutano  mkubwa kwa wataalam mbambali, Wataalamu ambao wametafautiana nasa katika mitazamo yao  na maoni yao kuhusu juu ya suala zima la asli na chimbuko la luhga ya Kiwsahili, na mivutano hiyo imepelekea kuibuka kwa nadhariya mbali mbali zinazoelezea asili na chimbuko la lugha ya Kiwsahili. Miongoni mwa nadhariya hizo ipo inayodai kuwa lugha ya Kiswahili ni lugha ya Upwa wa Afrika Mashariki. Kabla ya kujadili nadharia hii kwanza tutaangalia fasili ya Upwa wa Afrika Mashariki:
Upwa wa Afrika Mashariki  ni  maeneo ya pwani ya mwambao wa Afrika Mashariki  wenye urefu wa kilomita 1500km kuanzia pembe ya Afrika(Somalia) hadi kuteremkia Kaskazini mwa Msumbiji  pamoja na visiwa vyote vilivyopakana na mwambao wa Afrika Mashariki. (Shihabuddin & Mnyampala).
Lugha ya Kiswahili ni lugha ya Upwa wa Afrika Mashariki, wananadhariya wa nadhariya hii wanadai  kuwa lugha ya Kiswahili  asili na chimbuko lake hasa ni kutoka katika maeneo ya Upwa wa Afrika Mashariki kuanzia Somalia, Kenya, Tanzania hadi kaskazini ya Msumbiji.
Wananadhariya wa nadhariya hii wameeleza kuwa Kiswahili kimechimbukia katika maeneo tafauti ya Upwa wa Afrika ya Mashariki kuanzia Mogadishu, Lamu, Mombasa, Tanga, Dar es salaam, Kilwa, Mofia, Pemba hadi kaskazini ya Msumbiji. Kwa kuthibitisha dai hili tutafafanua kwa tupitia Ushahidi wa Kijografia, ushahidi wa Kilughawiya, Ushahidi wa Kihistoria na Ushahidi wa kiutamaduni.
Kwa kuanzia na Ushahidi wa kijografiya, katika ushahidi huu tutajikita zaidi katika kuangalia  ni maeneo yepi hasa duniani, lugha ya Kiswahili inazungumzwa na kutumiwa kwa sana na wakazi wake, ni wazi kuwa  maeneo ambayo  Kiswahili kinazungumzwa na kutumiwa kwa wingi zaidi ni katika maeneo ya Upwa wa Afrika Mashariki ambapo katika maeneo hayo wakaazi wake hutegemea na kutumia Kiwsahili kama ni Lugha ya kwanza katika shughuli zao zote. Hivyo ushahidi huu unatuthibitishia wazi kuwa chimbuko la Kiwsahili ni maeneo ya Upwa wa Afrika Mashariki, kwani kitu au jambo lolote lile pale kinapoanzia huwa kinapatikana kwa wingi kuliko zile sehemu kiliposambaa.
Ushahidi wa Kilughawiya, katika ushahidi huu tutajikita zaidi katika kuangalia Idadi ya wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili, Ufasaha wa lugha na Mfanano wa lahaja mbali mbali zinazopatikana katika Upwa wa Afrika Mashariki.
            Idadi ya wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili. Ni ukweli uliowazi kabisa kwamba idadi kubwa ya watumiaji na wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili duniani inapatikana katika maeneo ya Upwa wa Afrika ya Mashriki, kwani wenyeji wa maeneo haya hukitumia Kiswahili kama ni lugha yao ya kwanza na vile vile wenyeji wa maeneo haya hawana lugha nyengine badala ya Kswahili yaani hawana lugha za kimakabila hivyo sifa hii imeweza kuwatafautisha wenyeji wa asili wa Upwa wa Afrika Mashariki na wazungumzaji wa Kiswahili wa maeneo mengine duniani. Hivyo hoja hii inathibitisha kuwa Kiswahili kimeanzia katika maeneo ya Upwa wa Afrika Mashariki.
            Ufasaha wa lugha.Wenyeji asili wa Upwa wa Africa Mashariki huzungumza Kiswahili kwa ufasaha zaidi yaani kwa usahihi kuliko wazungumzaji wa Kiswahili wa maeneo ya ndani ya bara la Afrika na maeneo mengine duniani. Hivyo hii inatuthibitishiya kuwa lugha ya Kiswahili kimeazia katika Upwa wa Afrika ya Mashariki.
            Mfanano wa lahaja za mwambao wa Afrika Mashariki. Lahaja mbali mbali zinazopatikana katika mwambao wa Afrika Mashariki kwa kiasi kikubwa zinafanana katika matamshi na msamiati, lahaja hizo ni kama vile Kimtangata, Kitikuu, Kivumba, Kihadimu, Ki-Unguja mjini, Kitumbatu, Kipemba, Kimvita na Chi-miini.
Mfano I:          KIVUMBA                                KI-UNGUJA MJINI
                        Baka                                        Paka
                        Beleka                                     Peleka
                        Bika                                         Pika

Mfano II:         KI-UNGUJA                              KI-AMU                                   
                        -vunja                                      -vunda
                        Mchanga                                 mtanga
                        Chukua                                    tukua

Mfano III:        CHI-MIINI                                KI-MVITA
                        -aanza                                     -anda
                        Mapenzi                                  mapendi
                        Luma                                       lima
Kwa hiyo, kutokana na mfanano wa lahaja hizo  ni wazi kuwa lugha hizi zinatokana na msingi mmoja na chimbuko lake ni maeneo ya mwambao wa Afrika ya Mashariki.
Ushahidi wa kihistoriya.Katika ushahidi huu tutawazungumzia wageni mbali mbali ambao waliowahi kutembelea maeneo tafauti tafauti ya Upwa wa Afrika katika karne za mwanzo na  kuweza kutaja majina ya vitu mbali mbali  kwa lugha ambayo iliyokuwa ikizungumzwa na wenyeji wa mwambao wa Afrika Mashari katika maandishi yao. Miongoni mwa wanahistoria hao ni:
            Ali – Idrisa (1100 - 1160). Mgeni huyu alitembelea maeneo ya Zanzibar yaani Unguja, katika maandishi yake alitaja majina ya vitu mbali mbali ambavyo villivyopatikana katika maeneo ya Zanzibar, mfano; kikombe, mkono wa tembo, muriami na kisukari.
            Freeman Greville. Huyu ni mtaalam wa kihistoriya, katika makala yake ya “Medieval Evidence for Swahili” amelezea historia ya  miji mbali mbali inayopatikana katika mwambao wa Afrika Mashariki ukiwemo mji wa Kilwa, katika mji huu alitaja majina ya utani ya Wafalme wa kipindi hicho, kama vile nguo nyingi, Mkoma watu na Hasha hazimfiki.
Maelezo haya ya wanahistoriya yanaonesha kwamba lugha ya Kiswahili ilikuweko na wakaazi wa mwabao wakiitumia lugha hiyo tokea karne za mwanzo hata kabla ya kuja kwa wageni katika Upwa wa Afrika Mashariki, hivyo inathibitisha wazi kuwa lugha ya Kiswahili ilichimbukia katika maeneo ya Upwa wa Afrika Mashariki hata kabla ya ujio wa wageni.
Ushahidi wa Kiutamaduni. Katika ushahidi huu tutazungumzia shughuli za kiushumi katika jamii ya Waswahili. Kuna maandishi mengi ya Kihistoriya ambayo yameleza kuwa shughuli kuu ya kiuchumi iliyokuwa ikifanya naWaswahili ni shughuli za uvuvi. Hivyo tunaporudi na kuziangalia jamii zinazoishi katika Upwa wa Afrika Mashariki tuaona kuwa wenyeji wa maeneo hayowanajishughulisha zaidi na uvuvi kwa sababu wamezungukwa na bahari ya Hindi. Kwa hiyo tuaweza kuthubutu kusema kuwa, wenyeji wa Upwa wa Afrika Mashariki ndio Waswahili na lugha ya Kiswahili asili yake na chimbuko lake ni maeneo hayo ambayo manayoishi Waswahili.
UDHAIFU WA NADHARIYA
Kwanza, nadhariya hii imeshindwa kuainisha(kutaja) eneo mahsusi ambapo Kiswahili kimechimbukia au kuanzia ndani ya Upwa wa Afrika Mashariki.
Vile vile, nadharia hii imekosa mtaalam hata mmoja aliyefanya utafiti wa kina kwa kutoa vyanzo na ushahidi utakao tumika kuthibitisha dai hili kuwa Kiswahili ni lugha ya Upwa wa Afrika Mashariki.
            UBORA WA NADHARIYA
Nadharia hii imepelekea watalaam tafauti tafauti kuanza kufanya tafiti kina juu ya kuchunguza na kuthibitisha hoja mbali mbali zinazohusiana na historiya ya lugha ya Kiswahili.
Pia nadharia hii imeweza kuonesha ukweli juu ya chimbuko la lugha ya Kiswahili, kwani hoja zilizotumika kuthibitisha dai hili ni hoja za kimantiki yaani ni hoja zenye kuingia akilini.
           

Kwa ujumla,asili na chimbuko la lugha ya Kiswahili ni maeneo ya  Upwa wa Afrika Mashariki, ingawa kuna udhaifu wa hapa na pale lakini hoja zilizotumika kuthibitishia nadhariya hii ni hoja za kimantiki na zenye kukubalika kwa mwenye taaluma yoyoe yule.

No comments:

Post a Comment